SHINYANGA WAKAMATWA WAGANGA WA JADI WANAOSABABISHA MAUJA YA KIKATILI, VIFAA TIBA VYA HOSPITALI, KAMANDA MAGOMI TUMEFANYA MISAKO NA DORIA - TANZANIA NEWS

Breaking

HABARI ZA UKWELI

Monday, February 27, 2023

SHINYANGA WAKAMATWA WAGANGA WA JADI WANAOSABABISHA MAUJA YA KIKATILI, VIFAA TIBA VYA HOSPITALI, KAMANDA MAGOMI TUMEFANYA MISAKO NA DORIA

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limefanikiwa kukamata mali na vielelezo mbalimbali ikiwemo lita 780 za mafuta ya Disel, vifaa tiba vya Hospitali pamoja na waganga wa jadi wakiwa na vifaa vinavyotumika katika kupiga ramli chonganishi.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, Kamanda wa jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kamishna msaidizi wa Polisi Janeth Magomi amesema katika kipindi cha mwezi mmoja kuanzia Februari 5,2023 hadi Februari 27,2023 jeshi hilo limefanya misako na doria katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Shinyanga.

Kamanda Magomi amesema jumla ya waganga watatu wa jadi wamekamatwa wakiwa na vifaa vinavyotumika katika kupiga ramli chonganishi ambayo hupelekea mauaji ya kikatili huku akitaja mali na vielelezo mbalimbali vilivyokamatwa.

“Tumekamata jumla ya lita 780 za mafuta aina ya Disel katika maeneo tofauti ya mradi wa Reli ya mwendokasi SGR, Tumekamata waganga watatu wa jadi wakiwa na vifaa vinavyotumika katika kupiga ramli chonganishi ambayo hupelekea mauaji ya kikatili kama vile mauaji ya kutumia mapanga, tumekamata vifaa tiba vya Hospitali vya aina mbalimbali ambavyo haviruhusiwi kumilikiwa na mtu pasipo na idhini ya serikali, tumekamata pikipiki tatu zilizokuwa zinatumika katika uhalifu ikiwemo kubeba mafuta ya wizi katika mradi wa Reli yay a mwendokasi ya SGR”.amesema Kamanda Magomi

“Vitu vingine tulivyokamata na pamoja na milango tisa(9) ya chuma, mabomba matatu, ya chuma, bomba moja la alama za barabarani, tumekamata milango mitano (5) ya mbao mzani wa kupima uzito, mashine ya kutobolea miamba, Godoro moja vitu 4 vya plastick, ngoma moja ya shule na magitaa mawili”.amesema Kamanda Magomi

Kamanda Magomi ameeleza kuwa katika kipindi hicho jeshi hilo limefanikiwa kukamata bangi kete 31, mashine mbili za kuchezea kamali, Sub woofer mbili, feni moja, mtungi mmoja wa gesi pamoja na kuokoa pikipiki mbili.

Aidha Kamanda Magomi amefafanua jumla ya kesi 16 zilizopata mafanikio kwenye Mahakama ikiwemo kesi nane (8) za makossa ya wizi ambazo zilihukumiwa kati ya  kifungo cha Miezi mitatu hadi Miaka mitatu (3).

“Kesi nne za wazazi kutowapeleka watoto shule ambao wao walihukumiwa kulipa faini ya shilingi laki moja kila mmoja, kesi moja ya kujihusisha na vitendo vya ushirikiana ilihusisha kwenda jela miezi 6, kesi moja ya kutotii amri halali ya serikali ilihukumiwa kulipa faini ya shilingi laki moja na kesi moja ya kuingia kwa jinai ililipwa faini ya shilingi laki mbili lakini pia kesi moja ya kupatikana na mali idhaniwayo ya wizi ilihukumiwa kulipa faini ya shilingi laki tatu”.amesema Kamanda Magomi

Kamanda wa jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kamishna wa Polisi Janeth Magomi ametumia nafasi hiyo kuwapongeza wakazi wa Mkoa wa Shinyanga kwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo ili kuzuia uhalifu na wahalifu.

Kamanda Magomi amewaomba wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kuendelea kulipa ushirikiano jeshi la Polisi ili kutokomeza uhalifu huku akiwataka kuacha mara moja baadhi ya askari wanaovujisha siri na wengine kushirikiana na wahalifu na kusababisha kudhoofika kwa upatikanaji wa taarifa za kihalifu kutoka kwa wananchi ambapo amesema hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yao.

No comments:

Post a Comment

TANZANIA NEWS

TANZANIA NEWS
Habari za Ukweli

HABARI

SERIKALI YAFANIKIWA KUDHIBITI UGONJWA WA MARBURG ULIORIPOTIWA KAGERA

Na Mapuli Misalaba Serikali imefanikiwa kudhibiti ugonjwa wa   MARBURG ulioripotiwa katika Wilaya ya Bukoba Mkoani Kagera kuwa jumla ya wa...